Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai 31, 2021
Picha
kessyngocho.blogspot.com Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 1, 2021  Good morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam leo August 1, 2021,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za Magazeti ya Tanzania.
Picha
kessyngocho.blogspot.com Habari za moja kwa moja Maelezo zaidi kuhusu taarifa hii Habari za moja kwa moja Imepakiwa mnamo 19:18 30 Julai 2021 19:18 30 Julai 2021 Tanzania yapokea ndege ya tisa aina ya Bombardier Ikulu Tanzania Copyright: Ikulu Tanzania Tanzania imepokea ndege nyingine ya masafa ya kati aina ya Bombardier Dash 8- Q 400 kutoka nchini Canada. Ndege hiyo ilipokewa na Rais Samia Suluhu Hassan aliyewaongoza viongozi mbalimbali na baadhi ya watanzania waliojitokeza katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere. Hiyo ni ndege ya tisa kati ya 11 zinazotarajiwa kununuliwa na serikali kufikia mwaka 2022, ndege nyingine inatarajiwa kuwasili mwezi Oktoba mwaka huu. Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt Leonard Chamuriho ndege iliyopokelewa leo ni ya 5 ya masafa mafupi kununuliwa na Tanzania tangu mchakato wa kufufua Shirika hilo uanze katika kipindi cha miaka 5 iliyopita. Akizungumza wakati wa kupokea ndege hiyo, Rais wa nchi hiyo, Samia Suluhu alisema mbali na ndege za abiria nchi hiyo
Picha
kessyngocho.blogspot.com Chanzo kifo cha Babu wa Loliondo “hakutaka wajue anaugua” (+video) Pascal Mwakyoma TZA   Chanzo cha kifo cha Mchungaji Ambilikile Mwasapile (86) kimetajwa aliugua nimonia kali ambayo ilimsababisha kupata tatizo la upumuaji na homa. Tangu afariki wasaidizi wake na majirani wamekuwa wakieleza kushtushwa na kifo hicho ambacho kimetokea akiwa anaendelea kutoa huduma ya tiba ya kikombe aliyoanza tangu mwaka 2011. Mchungaji Ambilikile ambaye ataendelea kukumbukwa kwa kuvutia maelfu ya watu ndani na nje ya nchi kati ya mwaka 2011 hadi 2013 kutokana na tiba yake ya kikombe alifariki jana saa 9:45 jioni. Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mangwala amesema kuwa taarifa za awali za madaktari zinaeleza chanzo cha kifo ni nimonia ambapo kwa takriban siku tano alikuwa anaumwa na kupata sindano za masaa.