Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 17, 2021

Habari kutoka millardayo

Sharifat Hytham  ni mtoto wa Kitanzania mwenye  miaka 8  akiwa anasoma  Darasa la 4 katika Shule ya  Yemen  Dar es Salaam.  Ayo TV na Millardayo.com  imekutana na Sharifati ambae ana uwezo wa hali ya juu unaowashangaza wengi ikiwemo kuwaombea watu Dua, kuwafundisha Wanafunzi wenzake waliomzidi umri na kidato.   ‘ Naitwa Sharifat Hytham nasoma katika shule ya Yemen Primary, mimi ni mtoto wa kwanza katika familia yetu upande wa Mama na nina mdogo wangu wa kiume, muda ninaopata kusoma ni muda wa kukaa pekee yangu jioni tulivu pia nina muda wa kuwafundisha wenzangu kwa kipawa nilichopewa  na Mwenyezi  Mungu amenipa wepesi na amenijaalia wa kuwafundisha wenzangu walionivuka Madarasa na kiumri’- Sharifat Hytham